Sunday, February 17, 2013

KARZAI APIGAA MARUFUKU MASHAMBUIZI YA ANGA YANAYOFANYWA NA NATO


Rais Hamid Karzai wa Afghanistan amesema atatoa dikrii ya kupiga marufuku vikosi vya usalama vya nchi hiyo vinavyofanya operesheni katika maeneo ya raia kuomba msaada kwa vikosi vya NATO ili kutekeleza mashambulio ya anga katika maeneo hayo. Karzai ametoa tamko hilo leo zikiwa zimepita siku tatu tu tangu raia kumi walipouawa katika shambulio la anga lililofanywa na NATO mashariki mwa nchi hiyo. Mashambulio ya anga ya Shirika la Kijeshi la NATO na vifo vya raia vinavyosababishwa na mashambulio hayo yamepelekea kuzuka mkwaruzano kati ya Rais wa Afghanistan na vikosi vya kigeni vinavyomsaidia katika vita dhidi ya wanamgambo wa Taliban. Akihutubia hadhara ya maafisa, makomando na wanafunzi wa Akademia ya Taifa ya Kijeshi mjini Kabul Karzai amesema atatoa dikrii hiyo hapo kesho na kwamba kuanzia hapo vikosi vya usalama vya Afghanistan havitoweza katika hali yoyote ile kuviomba vikosi vya kigeni vifanye shambulio la anga kwenye maeneo ya nyumba na vijiji wakati wa operesheni za vikosi hivyo. Watu kumi wakiwemo watoto watano na wanawake wanne waliuawa siku ya Jumatano wakati makombora ya ndege za vikosi vya NATO yalipolenga nyumba mbili kwenye eneo la Shultan huko katika mkoa wa Kounar mashariki mwa Afghanistan.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO