Sunday, February 17, 2013

PAKISTAN YAOMBOLEZA MAUAJI YA WATU 81

Idadi ya vifo kufuatia shambulizi kubwa la bomu lililofanywa dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia kusini magharibi ya Pakistan imepanda leo na kufikia watu 81. Wakaazi wa eneo hilo wametishia kufanya maandamano ikiwa hakuna hatua madhubuti itakayochukuliwa dhidi ya waliofanya shambulio hilo. Bomu hilo lililokuwa na takribani tani moja ya miripuko, na kufichwa ndani ya tangi la maji, liliripuka jana jioni, katika soko moja lillokuwa limejaa watu katika mji wa Hazara, ambao unakaliwa na waislamu wengi wa Kishia. Eneo hilo liko karibu na Quetta; mji mkuu wa mkoa wa Baluchistan. Afisa mkuu wa polisi eneo hilo amesema idadi ya waliojeruhiwa imefika watu 178. Mkoa wa Baluchistan umeendelea kukumbwa na mashambulizi za kimadhehebu baina ya waislamu wa madhehebu ya Sunni walio wengi nchini humo, na washiya ambao wanajumlisha moja juu ya tano ya jumla ya watu milioni 180 nchini Pakistan. Shambulizi hilo la Jumamosi limefanya idadi ya mauwaji ya mashambulizi la kimadhehebu mwaka huu nchini Pakistan kufikia 200, ikilinganishwa na zaidi ya 400 waliouawawa mwaka wa 2012, mwaka ambao Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch liliztaja kuwa mbaya zaidi dhidi ya Washiya nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO