Sunday, February 17, 2013

RUSSIA YASEMA MRIPUKO ULIODHANIWA NI KIMONDO NI MAJARIBIO YA SILAHA ZA MAREKANI


Mjumbe mmoja katika bunge la Russia amesema mlipuko wa kimondo (meteor strike) uliojiri hivi karibuni katika eneo la milima ya Ural nchini humo ulikuwa jaribio la silaha mpya za Marekani.
Mbunge mashuhuri Vladimir Zhirinovsky amesema kinyume na inavyodhaniwa kilichoshuhudiwa  eneo la Ural si jiwe la nyota bali ni Wamarekani waliokuwa wakifanyia majaribio silaha zao mpya. Amedai kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry amekuwa akitaka kuzungumza na mwenzake wa Russia Sergei Lavrov bila mafanikio lengo likuwa ni kumuonya kuhusu kadhia hiyo. Siku ya Ijumaa kimondo kuliripuka angani na baadhi ya vipande kuporomoka katika eneo la Ural ambapo watu zaidi ya 1,200 walijeruhiwa. Aghalabu walipata majeraha kutokana na gilasi za madirisha  yaliyovunjika kutokana na nguvu ya mripuko mkubwa uliojiri katika tukio hilo.
Maafisa wa Wizara ya Maafa Russia wamesema wangali wanalitafuta jabali ambalo lililoporomoka kutoka angani na kuanguka katika Ziwa Chbarkul  lililoganda barafu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO