Sunday, February 17, 2013

KATIBU MKUU WA HIZBUL LAH ATANGAZA MSIMAMO WAO DHIDI YA ISRAEL


Kufuatia vitisho vinavyooengezeka kila uchao vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Lebanon na kukiuka mara kwa mara utawala huo ardhi ya Lebanon, Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Lebanon Hizbullah ameitahadharisha Tel Aviv juu ya madhara ya hatua zozote za hujuma dhidi ya ardhi ya nchi hiyo. Katika hotuba yake kwa mnasaba wa kukumbuka kuuawa shahidi viongozi wa muqawama wa Lebabon dhidi ya Israel, Sayyid Hassan Nasrullah jana alisema kuwa, viwanja vya ndege, bandari na vituo vya umeme vya utawala wa Kizayuni vinaweza kulengwa na makombora na roketi za Hizbullah, na kwamba mahesabu yoyote ya kimakosa ya viongozi wa Israel yanaweza kupelekea kuangamizwa kwao. Kuhusiana na kuunga mkono muqawama wa Palestina Sayyid Nasrullah amesema, muqawama nchini Lebabon unaunga mkono nguvu za wananchi wa Palestina na kwamba Wazayuni waliozikalia ardhi za Palestina kwa makumi ya miaka, katika siku za hivi karibini wataangamia. Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa, muqawama umeleta mafanikio makubwa nchini humo na kwamba katika mwaka uliopita umefanikiwa kubadilisha uwiano ambapo kwa miaka kadhaa iliyopita madola ya kibeberu yalikuwa yakiathiri mazingira ya eneo hilo.
Bila shaka kusimama kidete wananchi wa Lebanon dhidi ya Wazayuni kwa uongozi wa Harakati ya Hizbullah kumejenga ngome imara dhidi ya uchokozi wa utawala wa Kizayuni. Suala linalopaswa kukumbushwa hapa ni kuwa, kila siku maqawama unazidi kupendwa na wananchi wa Lebanon na fikra za waliowengi katika eneo huku suala hilo likipewa kipaumbele na viongozi wa nchi hiyo. Harakati ya muqawama nchini Lebanon iliyopelekea kushindwa mara kadhaa utawala wa Kizayuni katika miaka kadha iliyopita, inabainisha mabadiliko ya uwiano yaliyoshuhudiwa kutoka upande wa viongozi wa Tel Aviv na washirika wao katika eneo. Israel na washirika wake kwa kuendeleza siasa za kuzusha wasiwasi na woga katika eneo na kuongopa kwamba utawala huo hauwezi kushindwa, wamekuwa wakikusudia kuangamiza muqawama mkabala na kujipanua utawala huo na madola ya kibeberu katika Mashariki ya Kati. Lakini kushindwa utawala huo kutokana na kusimama kidete wananchi wa Lebanon, ambako kulishuhudiwa wazi mwaka 2000 Miladia, kumekwamisha mipango na njama za Israel na Marekani dhidi ya Lebanon na eneo zima kwa ujumla. Kushindwa huko kulipelea Israel irudi nyuma kutoka katika maeneo ya Lebanon iliyokuwa ikiyakalia kwa mabavu mwaka 2000. Kushindwa Tel Aviv na muqawama kuliendelea kushuhudiwa katika vita vya siku 33 mwaka 2006 na hivyo kuvunja kabisa madai ya uongo ya kutoshindwa utawala huo katika medani ya vita. Hii ni katika hali ambayo, kushindwa Israel katika vita hivyo, kulikwamisha kabisa mpango wa kibeberu wa Marekani kwa ajili ya Masahariki ya Kati uliojulikama kama 'Mashariki ya Kati Mpya' uliokuwa ukifuatiliwa kwenye vita hivyo. Muqawama wa Lebanon umebadilika na kuwa kigezo cha mapambano ya mataifa ya eneo dhidi ya utawala wa Kizayuni, na ushindi wake umeongeza nguvu na matumaini kwa Wapalesina katika mapambanao yao dhidi ya adui Mzayuni. Uzoefu unaonesha kuwa, kusimama kidete na kuendeleza muqawama ndiyo njia pekee ya kukabiliana na siasa za kupenda kujitanua za Israel, kwani njia za suluhu hazijakuwa na faida yoyote zaidi ya kushadidisha siasa za kupenda kujitanua na jinai za utawala huo. Hii ndio sababu Sayyid Hassan Nasrullah sambamba na kubainisha wazi kuwa aduia mkuu wa wananchi wa eneo la Mashariki ya Kati ni Israel na washirika wake, akasisitiza udharura wa kudumishwa muqawama na kusimama kidete dhidi ya Wazayuni.    
Na Fatma Muhammad Mbepey

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO