Thursday, February 21, 2013

LARIJANI ASEMA IRAN HAITAACHA KUIUNGA MKONO IRAN

Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu yaani Bunge la Iran amesema kuwa, kuuliwa kamanda wa ngazi ya juu wa vikosi vya Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) hakutaathiri uungaji mkono wa Iran kwa Lebanon. Larijani amesema hayo leo na kuongeza kuwa, maadui wanapasa kufahamu kwamba Iran haitaacha kuliunga mkono taifa la Lebanon kutokana na kuuawa Jenerali Hassan Shateri. Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran ametilia mkazo kwamba Iran itaendelea kuiunga mkono Lebanon kwa ushupavu kabisa. Itakumbukwa kuwa kamanda mmoja wa vikosi vya Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu Jenerali Hassan Shateri alitoa huduma na kufanya juhudi kubwa katika kufanikisha ujenzi wa maeneo mbalimbali yaliyoharibiwa huko kusini mwa Lebanon kutokana na uvamizi na vita vya utawala haramu wa Kizayuni. Mwaka 2006 Israel ilianzisha vita dhidi ya Lebanon, vita ambavyo vilidumu kwa siku 33 na kuharibu miundo mbinu na majengo mengi ya kusini mwa nchi hiyo. Tangu wakati huo Iran imekuwa ikitoa msaada mkubwa katika juhudi za kuyajenga upya maeneo hayo yaliyoathiriwa na vita vya utawala ghasibu wa Kizayuni.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO