Thursday, February 21, 2013

MARZOUKI ATAFUTA SULUHU TUNISIA

Rais Moncef Marzouki wa Tunisia amekutana na viongozi wa chama tawala cha Ennahda kuzungumzia uteuzi wa waziri mkuu mpya wa taifa hilo baada ya kujiuzulu kwa kiongozi aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Hamadi Jebali. Ofisi ya rais nchini humo imethibitisha kuwa Marzouki amekutana na mwenyekiti wa Ennahda Rachid Ghannouchi pamoja na viongozi wa vyama vingine viwili vinavyounda serikali yake kujaribu kutafuta suluhu.
Kumekuwepo na wito kutoka mataifa mbalimbali yakiitaka Tunisia kuchukua hatua sahihi. Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Guido Westerwelle amesema ni muhimu viongozi wa taifa hilo wakazingatia kuutatua mzozo huo badala ya kuzozana. Tunisia imekumbwa na mzozo wa kisiasa tangu alipouawa kiongozi wa upinzani Chokri Belaid kilichofuatiwa na pigo la kujiuzulu kwa waziri mkuu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO