Sunday, February 24, 2013

RAISI WA MISRI ABADILI TAREHE YA UCHAGUZI BAADA YA KULALAMIKIWA

Rais Mohammed Mursi  wa Misri amebadilisha ratiba ya uchaguzi wa bunge kufuatia malalamiko ya jamii ya wachache ya wakristo.Kwa mujibu wa televisheni ya taifa, uchaguzi huo uliopangwa kufanyika kwa awamu nne,utaanza hivi sasa April 22 na 23.Hapo awali uchaguzi huo ulipangwa kuanza April 27/28 na kwa namna hiyo ungefanyika wakati wa sherehe za pasaka za jamii ya wakristo wa madhehebu ya Koptik.Jamii hiyo inafikia asili mia 10 ya wananchi jumla wa Misri.Kwa jumla zoezi la uchaguzi litafanyika kwa awamu tofauti kote nchini humo na kuendelea hadi mwezi June mwaka huu.Kubadilishwa tarehe ya kupiga kura hakutaubadilisha wito wa upande wa upinzani kuususia uchaguzi huo.Upande wa upinzani unataka uchaguzi usiitishwe na badala yake iundwe serikali ya mpito itakayozijumuisha pande zote za kisiasa za nchi hiyo.Fikra hiyo inapingwa na chama cha Udugu wa kiislam cha rais Mohammed Mursi.Bunge la awali la Misri lilivunjwa mwezi June mwaka jana,miezi mitano tu baada ya kikao chake cha kwanza,baada ya korti ya katiba kusema uchaguzi haukuambatana na katiba.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO