Thursday, February 21, 2013

UFARANSA YATUMIA SILAHA ZA ISRAEL HUKO MALI


Ufaransa inatumia ndege zisizo na rubani (drone) zilizotengenezwa Israel katika vita vyake dhidi ya watu wa Mali.
Kwa mujibu wa jarida la World Tribune, Jeshi la Ufaransa linatimua drone aina ya “Harfang” iliyotengenezwa Israel. Drone hiyo inatumiwa kuvurumisha makombora katika maeneo ya kaskazini mwa Mali.
Ufaransa ilianzisha vita dhidi ya Mali Januari 11 mwaka huu kwa kisingizio cha kupambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo.  
Wakati huo huo Rais Francois Hollande wa Ufaransa ametangaza kuwa, komandoo mmoja wa jeshi la nchi yake ameuawa kwenye mapigano ya kaskazini mwa Mali. Komandoo huyo aliuawa kwa kupigwa risasi na waasi wa Ansaru Din katika milima ya Iforhas. 
Ufaransa inadai kuwa imeingia Mali kupambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo. Hata hivyo weledi wa mambo wanasema lengo kuu la hujuma ya Ufaransa huko Mali ni kupora utajiri wa nchi hiyo hasa mafuta ya petroli, dhahabu na madini ya urani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO