Saturday, February 23, 2013

URUSI YAISHUTUMU MAREKANI JUU YA SYRIA

Urusi imeituhumu Marekani kuwa ni ndumilakuwili juu ya mzozo wa Syria ikisema kuwa nchi hiyo imezuia kutolewa kwa tamko la baraza la usalama la Umoja wa Mataifa la kulaani mashambulizi ya hivi karibuni yaliyotokea jana mjini Damascus. Akiukosoa msimamo wa Marekani waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov, amewaambia waandishi wa habari kuwa wanaamini kwamba kitendo hicho cha Marekani ni aina ya undumilakuwili. Jana kulifanyika mashambulizi katika eneo la katikati la Damascus ambayo yaliuwa watu 53 karibu na ubalozi wa Urusi nchini Syria eneo ambalo pia ni makao makuu ya chama tawala cha Baath. Makundi ya wanaharakati yanaarifu kuwa watu waliokufa ni 83. Mashambulizi hayo yanaaminika kufanywa na waasi ambapo nao wameitupia lawama serikali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO