Thursday, March 28, 2013

IRAN YATAKA KUDHIBITIWA UUZAJI WA SILAHA


Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tehran inaunga mkono Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Biashara za Silaha unaolenga kudhibiti biashara ya silaha duniani.
Ahmadinejad ameyasema hayo Jumatano katika mazungumzo ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon. Rais Ahmadinejad amesema Iran ni muhanga wa ugaidi na hivyo inaunga mkono kikamilifu mkataba huo.
Rais wa Iran amesema kudhibiti usafirishaji silaha duniani ni jambo linaloweza kusaidia usalama wa kimataifa. Aidha ametaka hatua zichukuliwe kuboresha rasimu ya mkataba huo.
Kongamano la rasimu hiyo linaendelea leo Alkhamisi katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo kutafanyika juhudi za kudhibiti biashara ya silaha duniani inayokadiriwa kugharimu dola bilioni 70 kwa mwaka. Katika kikao cha Julai 2 hadi 27 mwaka uliopita, nchi wanachama hazikuweza kufikia mwafaka kuhusu rasimu hiyo. Mkataba huo unalenga kuweka viwango vipya vya uuzaji silaha kimataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO