Thursday, March 28, 2013

WAPINZANI WA SYRIA WAFUNGUA UBALOZI WAO WA KWANZA QATAR

Upinzani wa Syria unaotambuliwa kama mwakilishi halali wa watu wa Syria na Jumuiya ya n´Nchi za Kiarabu, umefungua ubalozi wake wa kwanza nchini Qatar jana Jumatano, katika pigo la kidiplomasia kwa utawala wa rais Bashar al-Assad. Lakini kiongozi wa muungano wa upinzani huo, Ahmed Moazi al-Khatib, alitumia fursa ya kukata utepe wa kufungua ubalozi huo, ambao uko katika jengo tofauti na lile ulipo ubalozi wa serikali ya rais Assad,  kuelezea kukatishwa tamaa na kushindwa kwa mataifa makubwa kusaidia zaidi harakati za kumuondoa rais Bashar al-Assad. Al-Khatib ambaye alijiuzulu wiki hii kama kiongozi wa muungano wa taifa wa Syria, lakini anaendelea na wadhifa huo kama msimamizi, alizungumzia pia tofauti za ndani zinazoukabili muungano huo, na kusema kuwa njia pekee ya kusonga mbele ni kuwa kitu kimoja.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO