Wednesday, March 27, 2013

IRAQ YAPINGA WAASI WA SYRIA KUPEWA UANACHAMA

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Hoshyar Zebari amelaani hatua ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) ya kuwapa uanachama magaidi wa Syria kwenye jumuiya hiyo. Zebari amesema hatua hiyo inakiuka sheria na katiba ya Arab League. Akifafanua zaidi nukta hiyo, Hoshyar Zebari amesema wanachama wa jumuiya hiyo ni serikali za nchi za Kiarabu zilizochaguliwa kidemokrasia na wananchi na wala sio makundi yanayobeba silaha. Amesisitiza kwamba, magaidi wa Syria wanaungwa mkono zaidi na nchi za kigeni na hilo linakiuka vipengee muhimu vya mkataba wa kuundwa Jumuiya hiyo. Iraq ambayo kwa sasa ndiyo mwenyekiti wa kiduru wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imekuwa ikisisitiza kuwa njia pekee ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro wa Syria ni kupitia mazungumzo kati ya serikali na waasi. Radiamali ya Iraq inakuja siku moja baada ya Arab League kuchukua nafasi ya Syria katika jumuiya hiyo na kuwapa magaidi wanaopigana na serikali ya Rais Bashar Asad.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO