Wednesday, March 27, 2013

JESHI LA ISRAEL LAWAKAMATA VIONGOZI WA HAMAS

Jeshi la utawala haramu wa kizayuni wa Israel limewatia nguvuni viongozi 3 waandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS baada ya kushambulia makaazi yao katika mji wa Khalil. Habari zinasema kuwa, wanajeshi wa Kizayuni wamemtia nguvuni Mohammad Jamal mwenye umri wa miaka 55 baada ya kumvurugia nyumba yake na kuchukua vitu vyake vya kibinafsi zikiwemo kompyuta na simu ya mkononi. Wazayuni hao maghasibu pia wamewakamata Amjad Hamouri na Abdul-Khaliq Natshe na kuwapeleka katika eneo lisilojulikana. HAMAS imelaani hujuma hiyo na kusema inakiuka makubaliano ya usitishaji vita yaliyomaliza mapigano ya siku 8 kati ya pande mbili hizo mwaka uliopita. Utawala haramu wa Israel umeendelea kukiuka haki za wapalestina sambamba na kukanyaga sheria za kimataifa huku Jamii ya kimataifa ikiendelea kuwa kimya. Uungaji mkono wa hali na mali wa Marekani ndio sababu ya kuendelea kuvimba kichwa  utawala huo haramu wa Kizayuni.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO