Wednesday, March 27, 2013

RAIS WA SUDAN ATAKA WAASI KUSHIRIKI KATIBA MPYA

Makamu wa kwanza wa rais wa Sudan, Ali Osman Taha ametoa wito kwa makundi ya waasi kushiriki mchakato wa kuunda katiba mpya ya nchi hiyo. Katika hali isiyo ya kawaida, Taha amewakaribisha Malik Agar na Abdul-Aziz al-Hilu; viongozi wa kundi la waasi la SPLM-North na kusema kwamba, kushiriki kwao kwenye mchakatu wa kuandika katiba mpya utahitimisha fujo na tandabelua katika majimbo ya Blue Nile na Kordofan Kusini. Makamu wa kwanza wa rais wa Sudan aidha amesema katiba mpya itafungua milango ya kuelekea kwenye demokrasia halisi pamoja na kuleta amani na utulivu ndani na nje ya Sudan. Vita na rangaito katika mikoa ya Kordofan Kusini na Blue Nile vilianza punde baada ya Sudan Kusini kujitenga na Sudan mwezi Julai mwaka 2011 na nchi mbili hizo zimekuwa zikinyoosheana kidole cha lawama kuhusu uungaji mkono wa waasi katika majimbo hayo yaliyoko kwenye mpaka wao wa pamoja.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO