Wednesday, March 27, 2013

SHAMBULIO LA BOMU LAUA MMOJA RWANDA


Mripuko wa guruneti uliotokea mjini Kigali Rwanda umeua mtu mmoja na kuwajeruhi wengine wanane. Msemaji wa polisi ya Rwanda ameeleza kuwa guruneti hilo liliripuka jana jioni katika sehemu iliyoko baina ya kituo cha basi na soko moja kwenye eneo la Kimironko katika mji mkuu Kigali. Baadae polisi ilisema kupitia ukurasa wake wa twitter kwamba watu wawili wametiwa mbaroni kwa kushukiwa kutekeleza shambulio hilo. Itakumbukwa kuwa milipuko mingine mitatu ya maguruneti ilitokea nchini Rwanda katika kipindi kama hiki mwaka jana yaani katika mwezi Machi. Mlipuko mmoja wa guruneti uliua mtu mmoja na kuwajeruhi wengine watano huko kaskazini mwa Rwanda na milipuko mingine miwili  iliwajeruhi watu sita huko Kigali. Rwanda imekuwa ikikabiliwa na milipuko ya guruneti tangu mwaka 2010 huku serikali ikiwanyooshea kidole cha tuhuma maafisa wawili wa ngazi za juu wa jeshi la nchi hiyo waliokimbilia uhamishoni.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO