Saturday, April 20, 2013

AZERBAIJAN; HATUKUBALI KUTUMIKA ARDHI YETU KUISHAMBULIA IRAN

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa  Jamhuri ya Azerbaijan amesema kuwa, Baku haitakuwa kituo cha kijeshi cha Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusiana na uwezekano wa kufanyika shambulio la kijeshi  dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Elman Abdullayev ambaye hapo kesho ataongoza ujumbe wa nchi yake huko Tel Aviv ameongeza kuwa, serikali ya Azerbaijan inapinga chokochoko zozote zile dhidi ya Iran na kusisitiza kuwa, nchi hiyo kamwe haitakubali kutoa rufsa kwa Marekani na Israel kutumia ardhi yake  kuishambulia kijeshi Iran.  Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Azerbaijan ametaka kadhia ya nyuklia ya Iran itatuliwe kwa njia za kidiplomasia. Ameongeza kuwa, iwapo Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel zitaamua kuishambulia Iran, Jamhuri ya Azerbaijan haitaegemea upande wowote kwenye mgogoro huo, na wala haitakubali kutumiwa ardhi yake dhidi ya Iran.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO