Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya 
Lebanon imekanusha madai kuwa imetuma ndege isiyokuwa na rubani (drone) katika 
ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina huko Israel. Jeshi la utawala haramu 
wa Kizayuni jana lilitangaza kuwa, limetungua ndege isiyo na rubani inayodaiwa 
kumilikiwa na harakati ya Hizbullah ya Lebanon karibu na bandari ya kaskazini 
mwa Haifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Msemaji wa Jeshi la 
utawala huo alisema kuwa, ndege hiyo ilitambuliwa ikiwa katika anga ya Lebanon 
katika umbali wa kilometa nane kutoka pwani ya magharibi mwa Haifa na 
kudondoshwa na jeshi la Israel.
Katika upande mwingine Waziri wa Mambo ya Nje wa 
Lebanon amesema kuwa harakati ya Hizbullah haiingilii masuala ya Syria. Adnan 
Mansour amesema kwamba, askari wa Hizbullah wapo kwenye vijiji vya mpaka wa 
Lebanon kwa ajili ya kulinda Walebanoni wa eneo hilo na wala hawashiriki katika 
operesheni za kijeshi ndani ya Syria.
No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO