Friday, April 26, 2013

HIZBULLAH NAO WAKANUSHA JUU YA DRONE YAKE

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imekanusha madai kuwa imetuma ndege isiyokuwa na rubani (drone) katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina huko Israel. Jeshi la utawala haramu wa Kizayuni jana lilitangaza kuwa, limetungua ndege isiyo na rubani inayodaiwa kumilikiwa na harakati ya Hizbullah ya Lebanon karibu na bandari ya kaskazini mwa Haifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Msemaji wa Jeshi la utawala huo alisema kuwa, ndege hiyo ilitambuliwa ikiwa katika anga ya Lebanon katika umbali wa kilometa nane kutoka pwani ya magharibi mwa Haifa na kudondoshwa na jeshi la Israel.
Katika upande mwingine Waziri wa Mambo ya Nje wa Lebanon amesema kuwa harakati ya Hizbullah haiingilii masuala ya Syria. Adnan Mansour amesema kwamba, askari wa Hizbullah wapo kwenye vijiji vya mpaka wa Lebanon kwa ajili ya kulinda Walebanoni wa eneo hilo na wala hawashiriki katika operesheni za kijeshi ndani ya Syria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO