Friday, April 26, 2013

KOREA KUSINI YAONDOA WAFANYAKAZI WAKE KAESONG

Korea ya Kusini imesema itawaondoa wafanyakazi wake wote kutoka eneo la viwanda inalolimiliki pamoja na Korea ya Kaskazini. Uamuzi huo umefikiwa baada ya Korea ya Kaskazini kutupilia mbali pendekezo la Kusini, kuhusu mazungumzo juu ya kuanza tena kazi katika eneo hilo la viwanda la Kaesong.
Jana Korea ya Kusini iliipa Kaskazini muda wa masaa 24 kukubali pendekezo hilo, na kuonya kuwa endapo litakataliwa ingechukua hatua muhimu ambazo hata hivyo ilikuwa haikuzitaja. Eneo la viwanda la Kaesong linatoa ajira kwa wafanyakazi wapatao 53 elfu katika kampuni 123 za Korea ya Kusini. Eneo hilo ambalo liko umbali wa kilomita 10 ndani ya Korea ya Kaskazini, ni mfano adimu wa ushirikiano kati ya nchi hizo.
Korea ya Kaskazini iliwaondoa wafanyakazi wake wote tarehe 9 Aprili na kusimamisha shughuli zote, kudhihirisha hasira zake dhidi ya kauli ya Korea ya Kusini kwamba ingepeleka wanajeshi kulinda raia wake katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO