Friday, April 26, 2013

MUSHARAF AHUSISHWA NA KIFO CHA B.BUTTO

Jenerali Pervez Musharraf rais wa zamani wa Pakistan ametiwa mbaroni kuhusiana na kesi ya mauaji ya waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo Benazir Bhutto. Musharraf anatuhumiwa kula njama za mauaji ya Bi. Butto aliyefariki dunia katika shambulizi lililotokea Disemba mwaka 2007. Imeelezwa kuwa, Musharraf anaendelea kubakia nyumbani wake mjini Islamabad anakoshikiliwa kwenye kifungo cha nyumbani kutokana na uamuzi wake wa kuwatimua kazi majaji Novemba mwaka 2007 alipotangaza hali ya hatari nchini humo.
Kukamatwa kwake pamoja na kukosa sifa za kugombea uchaguzi wa Mei 11 vimetoa pigo kubwa kwa kiongozi huyo wa zamani wa kijeshi wa Pakistan, ambaye alirejea nchini humo mwezi uliopita akiahidi kile alichokiita kuwa ni 'kuiokoa' nchi. Inafaa kushiaria hapa kuwa, hadi sasa hakuna hata mtu mmoja aliyepatikana na hatia au kuhukumiwa kutokana na mauaji ya Bi. Benazir Bhutto, ijapokuwa kesi hiyo imekuwa ikiendelea kwa muda mrefu sasa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO