Tuesday, April 23, 2013

MPANGO WA KIGAIDI TORONTO

Polisi nchini Canada wamewafungulia mashitaka washukiwa wawili kwa kupanga njama ya kuiripua treni ya abiria katika eneo la Toronto. Njama hiyo kubwa ya shambulio la kigaidi imetibuliwa nchini humo kwa usaidizi wa maafisa wa usalama wa Marekani. Maafisa wa usalama wamesema wamekuwa wakiichunguza njama hiyo mjini Toronto na Montreal kwa mwaka mmoja sasa, na wamesema waripuaji hao wanadaiwa kuhusika na mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda. Washukiwa hao wawili sio raia wa Canada na polisi nchini humo hawajasema ni raia wa nchi gani. Naibu kamishna wa polisi nchini Canada, James Maliza amesema washukiwa hao hawakuwa karibu na kufanya shambulio hilo. Wanatarajiwa kufikishwa mahakamani leo. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO