Monday, April 22, 2013

MTAYARISHAJI WA FILAMU YA KIHOLANZI YA KUMKASHIFU MTUME ASILIMU

Moja ya wanachama wa chama cha Uhuru cha mlengo wa kulia chenye siasa kali nchini uhol...anzi Asilimu. Bwana Arnaud Fandor amesilimu na hivi karibuni katembelea Maka na Madina,baada ya kutoa mchango mkubwa katika kutengeneza filamu ya kumkashifu mtume rehema na amani ziwe juu yake.Gazeti la Okadh online la nchini Saudi arabi limeeleza kuwa liliongozana sambamba na bwana Arnaud Fandor pindi alipoutembelea msikiti wa mtume katika mji wa Madina.
Linasema ya kuwa Arnaud alilia sana pindi alipo litembelea kaburi la mtume rehema na amani ziwe juu yake.

Bwana Arnaud alisema ya kuwa:Hakika yeye alikuwa ni mwanachama wa chama chenye itikadi kali sana,chenye kuichukia dini ya kiislamu. Anasema pindi alipoona majibu ya waislamu dhidi ya filamu ile,akaamua kuanza kuusoma uislamu na kutaka kujua zaidi siri ya waislamu kuipenda dini yao na mtume wao kiasi hiki.
Bwana Arnaud anasema kuwa shughuli hii ya upekuzi wake juu ya uislamu iemepelekea kugundua ukubwa wa uovu ulio fanywa na chama chake cha zamani,akazidi vutika na uislamu na kutaka kujua zaidi juu ya uislamu kwa kuzidisha kusoma vitabu mbali mbali vya uislamu na kujiweka karibu na waislamu, mpaka akaamua kusilimu.Gazeti hilo pia limemalizia kwa kusema kuwa bwana Arnaud pia kautembelea mlima wa Uhudi. Aliye upande wa kulia katika picha ni bwana Arnaud akiwa radhwa sharifu ndani ya msikiti wa mtume.
 
 
Sources:
 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO