Iran na Russia zimetoa wito wa kufanyika 
mazungumzo bila masharti kama njia ya kuhitimisha mgogoro wa Syria uliopelekea 
maelfu ya watu kuuawa katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili sasa. Wito huo 
umetolewa katika mazungumzo kati ya Hussein Amir Abdollahian Naibu Waziri wa 
Mambo ya Nje wa Iran na mwenzake wa Russia Mikhail Bogdanov yaliyofanyika hapa 
mjini Tehran. Wawili hao walijadili pia njia za kusaidia pande za Syria 
kuanzisha mchakato wa kisiasa utakaoweza kusaidia kuhitimisha mapigano nchini 
humo.
Katika upande mwingine jeshi la Syria limedhibiti 
mji muhimu karibu na Damascus baada ya wiki kadhaa za mapigano na waasi 
wanaofadhiliwa kwa fedha na silaha na nchi za kigeni. Mji huo wa kistratejia wa 
Otaybah umedhibitiwa na jeshi la Syria baada ya mapigano makali yaliyopelekea 
waasi wengi kuuawa. Mji huo ulikuwa unatumiwa na waasi kupitishia s
No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO