Friday, April 26, 2013

RUSSIA NA IRAN ZATAKA SYRIA ISIWEKEWE MASHARTI KATIKA MAZUNGUMZO

Iran na Russia zimetoa wito wa kufanyika mazungumzo bila masharti kama njia ya kuhitimisha mgogoro wa Syria uliopelekea maelfu ya watu kuuawa katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili sasa. Wito huo umetolewa katika mazungumzo kati ya Hussein Amir Abdollahian Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran na mwenzake wa Russia Mikhail Bogdanov yaliyofanyika hapa mjini Tehran. Wawili hao walijadili pia njia za kusaidia pande za Syria kuanzisha mchakato wa kisiasa utakaoweza kusaidia kuhitimisha mapigano nchini humo.

Katika upande mwingine jeshi la Syria limedhibiti mji muhimu karibu na Damascus baada ya wiki kadhaa za mapigano na waasi wanaofadhiliwa kwa fedha na silaha na nchi za kigeni. Mji huo wa kistratejia wa Otaybah umedhibitiwa na jeshi la Syria baada ya mapigano makali yaliyopelekea waasi wengi kuuawa. Mji huo ulikuwa unatumiwa na waasi kupitishia s

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO