Friday, April 26, 2013

WALIOUWAWA BANGLADESH AJALI YA GHOROFA YAFIKIA 200

Maelfu ya Ndugu na jamaa ya Waathirika wa ajali ya kuanguka kwa jengo nchini Bangladesh waeshuhudia vikosi vya uokoaji vikiwatafuta wapendwa wao katika vifusi vya jengo hilo wakati huu ambapo idadi ya waliopoteza maisha imefikia takriban 200. Ajali hii imezua ukosoaji mkubwa dhidi ya makampuni ya magharibi kuwa yalikuwa yamewekwa mbele kuliko usalama kwa kuweka vyanzo vya bidhaa zao na kutengeneza nchini Bangladesh ingawa nchi hiyo imekuwa na Rekodi ya kupatwa na ajali za namna hiyo. Mamia ya Wafanyakazi walitoka katika viwanda vyao wakiandamana wakati bendera zikipepea nusu mlingoti ikiwa siku ya kitaifa kuomboleza kwa ajili ya wale waliopoteza maisha.
 Sauti za watu kadhaa walionusurika waliofunikwa na vifusi wakiomba msaada zimetoa matumaini lakini Wafanyakazi wa huduma za dharura wametumia siku nzima hii leo kutoa Miili ya Watu. Ajali ya kuanguka kwa jengo lililokuwa na kiwanda cha nguo imeashiria kuwepo kwa tatizo la usalama na Mazingira mabaya ya kufanya kazi vinavyokumba kiwanda hicho kilicho cha pili kwa biashara ya usafirishaji wa Bidhaa kwenda nje. Mwezi Novemba mwaka jana moto mkubwa ulisababisha watu 111 kupoteza maisha katika mji wa Dhaka .

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO