Tuesday, May 28, 2013

CHINA YAKANUSHA WIZI WA TAARIFA ZAMTANDAO ZA SHIRIKA LA KIJASUSI LA AUSTRALIA

Serikali ya Australia imeituhumu nchi ya China kwa kuhusika na wizi wa taarifa za siri toka shirika lake la kijasusi, waziri wa mambo ya kigeni wa Australia, Bob Carr amedhibitisha. Kwenye taarifa yake, waziri Carr amesema kuwa kufuatia uchunguzi walioufanya wamebaini kuwa maharamia waliovamia mtandao wa shirika la ujasusi wa nchi hiyo walitokea nchini China ambapo wamefanikiwa kuiba baadhi ya nyaraka na programu za vitarakilishi.
Waziri Carr ameongeza kuwa licha ya taarifa hiyo uhusiano baina ya mataifa hayo mawili utaendelea kusalia kama kawaida wakati huu ambapo wakifanyia kazi suala hilo ikiwemo kubaini waliohusika na uharamia. Tukio hili linatokea ikiwe umepita mwezi mmoja toka ikulu ya Marekani iituhumu nchini ya China kuhusika na wizi wa taarifa za Serikali yake tuhuma ambazo China imekanusha.
Tayari wizara ya mambo ya kigeni ya China imekanusha nchi yake kuhusika moja kwa moja na wizi wa taarifa za siri nchini Australia na Marekani na kwamba wanaofanya hivyo ni kikundi cha maharamia wachache walioko nchini mwake. Wataalamu wa masuala ya mtandao wanasema kuwa ni vigumu sana kwa sasa kuwabaini maharamia waliotekeleza wizi huo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO