Thursday, May 30, 2013

MSIBA MKUBWA: NDOA YA KWANZA YA JINSIA MOJA YAFUNGWA NCHINI UFARANSA


Baada ya sheria ya ndoa za jinsia moja kuhalalishwa nchini Ufaransa, ndoa ya kwanza yafungwa jana huko Montpellier, Ufaransa. Wakionekana kufurahia ndoa yao, Bwana Bruno Boileau anaeleza kuwa ana furaha kubwa kwa kufanikiwa kwa ndoa hiyo. Anaeleza sababu za kumpenda mwanaume mwenzake ambae kwa sasa ndio "Mke wake" aitwae Vincent Autin kwa ni mtu aneweza kumtuliza, mwenye mvuto, anayejitambua na mwenye matarajio makubwa. Nae bwana Vincent asema anampenda "Mume wake" kwasababu anamlinda vizuri na ndio mlinzi wake anaemtegemea. Bruno anasema kwa kujiamini, "tunataka tupate watoto na tunataka tuendeleze mila hii mpaka vizazi vijavyo". Nae Vincent anasema "Ufaransa leo imeturudishia haki yetu ya msingi ambayo tumezaliwa nayo". Na hapa ndipo ulimwengu ulipofikia, sijui huko tunakoelekea itakuaje???? 


No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO