Thursday, May 30, 2013

ISRAEL YAITISHA RUSSIA KUHUSU MAKOMBORA

Baada ya Russia kuamua kuiuzia Syria mitambo ya kisasa ya kuzuia makombora, Israel imeingiwa na kiwewe na kutoa vitisho dhidi ya Moscow kuhusiana na mpango wake huo ikisema kwamba, iko tayari kutumia mabavu kuzuia Syria kupelekewa makombora hayo. Jana Jumanne Russia ilitangaza kwamba itaendelea na mpango wake waliokubaliana na serikali ya Damascus wa kuipatia Syria mmitambo ya kuzuia makombora aina ya S-300, na kwamba suala hilo litazuia uingiliaji wa wageni katika masuala ya ndani ya Syria. Moshe Ya'alon Waziri wa utawala wa kizayuni wa Israel anayeshughulikia masuala ya kijeshi amedai kuwa, ni wazi suala hilo ni tishio kwao na kutishia kwamba iwapo silaha hizo zitaifikia Syria basi Israel itajua la kufanya

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO