Monday, May 27, 2013

JENERALI SEJUSA AOMBA ULINZI UINGEREZA

Jenerali wa jeshi la Uganda anayetafutwa na serikali ya nchi hiyo ameomba ulinzi wa polisi ya Uingereza na hatorudi nyumbani hivi karibuni. Joseph Luzige, wakili wa Jenerali David Sejusa, amesema Jenerali huyo hivi sasa amekuwa akijificha kuwakimbia makachero wa Uganda ambao inadaiwa kuwa wametumwa kwenda kumsaka akiwa safarini huko London Uingereza. Wakili huyo amesema Sejusa anayeongaza idara za usalama za ndani na nje ya Uganda anaamini kwamba maisha yake yako hatarini na kwamba amekuwa muangalifu sana. Hivi karibuni, jenerali huyo aliandika barua kwa idara ya usalama ndani ya nchi kutaka ufanyike uchunguzi juu ya repoti kuhusu mpango wa kumrithisha madaraka mtoto wa kiume wa Rais Yoweri Museveni ambapo wale wanaoupinga mpango huo wako katika hatari ya kuuwawa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO