Monday, May 27, 2013

UJERUMANI YAVUNJA REKODI YA KUUZA SILAHA NDOGONDOGO

Mauzo ya silaha ndogo ndogo za Ujerumani ya mwaka jana yanaripotiwa kuvunja rikodi ambayo haikuwahi kushuhudiwa hapo kabla. Kampuni za kutengeneza silaha za Ujerumani zimejipatia mapato makubwa zaidi hapo mwaka 2012 kutokana na mauzo ya silaha ndogo ndogo kuliko mwaka 2011 kwa mujibu wa Südeutscghe Zeitung. Kwa mujibu wa gazeti hilo mauzo ya silaha hizo zilizosafirishwa nje kwa mwaka 2012 yamefikia euro milioni 76.15 kulinganisha na euro milioni 37.9 kwa mwaka 2011. Kiwango kikubwa cha mauzo hayo kuwahi kurikodiwa katika ripoti ya serikali ya Ujerumani ya mauzo ya silaha ndogo nje ya nchi tokea mwishoni mwa miaka 1990, ilikuwa kuanzia mwaka 2009 ambapo yalifikia euro milioni 70.4. Gazeti hilo limesema limepata takwimu hizo kutoka kwa chama cha Linke cha sera za mrengo wa shoto. Bastola,bunduki nyepesi za rashasha,mabomu madogo kama yale yanayaoweza kurushwa kwa mkono na mabomu ya kutegwa ardhini ni miongoni mwa silaha zinazohesabiwa kuwa ndogo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO