Saturday, May 25, 2013

JESHI LA NIGERIA LAHARIBU KAMBI YA BOKO HARAM


Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, limeharibu na kudhibiti kambi kadhaa muhimu zilizokuwa zikitumiwa na kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Brigadia Christ Olukolade afisa wa habari wa jeshi hilo amesema, kambi hizo zilikuwa zikitumiwa katika kupanga operseheni za waasi na walikuwa wakishambulia maeneo ya karibu kutokea huko.
Wiki iliyopita askari 2,000 walipelekwa kwenye eneo hilo katika operesheni kubwa ya kupambana na kundi la Boko Haram.  Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria kutangaza hali ya hatari katika majimbo matatu ya kaskazini mashariki mwa nchi yanayohesabiwa kuwa ngome kuu ya kundi hilo. Wakati huo huo wanawake na watoto 6 waliokuwa wametekwa nyara na wanamgambo wa Boko Haram wameachiliwa huru.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO