Saturday, May 25, 2013

MACHAFUKO YAENEA NJE YA MJI MKUU WA SWEDEN


Machafuko yameenea nje ya mji mkuu wa Sweden Stockholm, ambako waandamanaji wamechoma moto magari na nyumba katika miji miwili ya nchi hiyo. Polisi imesema kuwa, waandamanaji wamechoma moto shule, majumba na magari kadhaa katika miji ya Oerebto na Sodertalje nje ya mji wa Stockholm. Wakati huo huo magari yameendelea kuchomwa katika vitongoji kadhaa vya wahamiaji kwa usiku wa 6 mtawalia wa machafuko yaliyoukumba mji mkuu wa Sweden, suala lililoilazimu polisi ya mji huo kuomba msaada.
Maandamano yalianza nchini Sweden May 19, siku 6 baada ya polisi kumpiga risasi na kumuua mwanaume wa miaka 69 nyumbani kwake kwenye eneo la wakaazi wengi masikini la Husby. Kitendo hicho kimeamsha hasira ya vijana wa eneo hilo wanaodai kwamba serikali inawabagua.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO