Monday, May 27, 2013

JESHI LA SYRIA LAZIDI KUWARUDISHA NYUMA WAASI

Pamoja na kuongezeka njama mbalimbali  za madola ya Magharibi kwa kushirikiana na baadhi ya nchi za eneo, dhidi ya Syria, jeshi la nchi hiyo limezidi kupiga hatua kubwa katika mapambano yake na waasi. Katika oparesheni za hapo jana katika maeneo tofauti ya nchi hiyo, waasi wanaoungwa mkono na Magharibi, utawala haramu wa Kizayuni na vibaraka wao wa eneo, walipata kipigo kikali kutoka kwa jeshi la Syria na wengi wao kuangamizwa.
Aidha jeshi hilo limefanikiwa kudhibiti asilimia 80 ya mji wote wa Al-Qusair kusini mwa nchi hiyo. Mbali na hayo, karibu waasi 50 waliokuwa wakipambana dhidi ya serikali halali ya Damascus katika maeneo tofauti ya nchi hiyo, ikiwemo Damascus, Idlib na Homs, wamejisalimisha kwa vikosi vya serikali. Suala hilo limezusha hofu kubwa katika safu za waasi na hivyo kuomba uungaji mkono zaidi wa kijeshi na kifedha kutoka kwa baadhi ya nchi za Kiarabu na za Magharibi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO