Monday, May 27, 2013

AL SHABAB WAZIDISHA MASHAMBULIZI NDANI YA KENYA

Watu wanane wameuawa baada ya wanamgambo wa kundi al al Shabab kufanya mashambulizi ndani ya ardhi ya Kenya. Sheikh Abdi Aziz abu Mas'ab Msemaji wa kundi la al Shabab amesema kuwa, kundi hilo limefanikiwa kuwauwa watu wanane baada ya kushambulia makao ya kijeshi katika eneo la Damajale nchini Kenya. Msemaji wa al Shabab ameongeza kuwa, kwenye shambulizi hilo, wanamgambo wa al shabab wamewateka nyara wanajeshi wawili wa Kenya. Viongozi wa Kenya wamethibitisha kutekwa nyara wanajeshi hao. Kabla ya hapo siku ya Jumamosi, wanamgambo wa al Shabab walishambulia kituo cha polisi kilichoko katika mji wa Liboi kwenye eneo la mpaka wa Kenya na Somalia na kusababisha watu sita kuuawa wakiwemo polisi wawili. Wakati huohuo, Rais wa Somalia amesema kuwa, kundi la al Shabab bado ni tishio katika eneo na ulimwenguni mzima. Rais Hassan Sheikh Mahmoud ameongeza kuwa, ijapokuwa kundi hilo limepoteza udhibiti wa maeneo mengi nchini humo, amma bado linaendeleza operesheni katika maeneo mbalimbali

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO