Saturday, May 04, 2013

NCHI KADHAA ZATAKA KUBADILISHWA MUNDO WA UN

Nchi kadhaa wanachama wa Umoja wa Mataifa zimetaka ubadilishwe  muundo wa umoja huo na badala yake kuwe na haki sawa kwa wanachama wote wa umoja huo. Mwakilishi wa Uswisi katika Umoja wa Mataifa akiwa mwakilishi wa kundi la zaidi ya nchi 15 kwenye umoja huo amesema kuwa, wanachama wa Umoja wa Mataifa ambao sio wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanapasa kuwa na haki zaidi kwenye umoja huo, na kusisitiza kwamba Umoja wa Mataifa unapasa kufanyiwa marekebisho ya kimsingi, kwani nchi zote wanachama wa umoja huo zinalazimika kutelekeza maazimio ya Baraza la Usalama. Nchi za Uswisi, Ireland, Uruguay, Norway na nchi nyingine 10 zimeunda kundi linalopigania haki sawa  kwenye umoja huo hata  kwa nchi zisizo wajumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama.  Kundi hilo pia limeeleza kuwa, kura ya veto si ya kisheria, kwani kwa miaka kadhaa sasa Washington imekuwa ikiitumia vibaya kura ya veto kwa kuukingia kifua utawala wa Kizayuni wa Israel.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO