Friday, May 24, 2013

LAGARDE ATINGA TENA MAHAKAMANO


Mahakama moja nchini Ufaransa inamuhoji kwa siku ya pili mfululizo Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF, Christine Lagarde, juu ya dhima yake katika kuagiza malipo ya mfanyabiashara mmoja hapo mwaka 2008 wakati akiwa waziri wa fedha wa Ufaransa. Lagarde aliandaa makubaliano ambayo yalipelekea kulipwa kwa fidia ya zaidi ya euro milioni 285 kwa Bernard Tapie. Fedha hizo zikijumuishwa na riba kwa jumla zinafikia euro milioni 400.Baada ya kusailiwa kwa masaa 12 hapo jana, mkuu huyo wa IMF amesema kikao hicho cha mahakama kingeliendelea leo hii. Mahakama hiyo haikutowa taarifa yoyote ile rasmi. Tapie ambaye alikuwa mmliki mkuu wa kampuni ya Adidas alidai kwamba alidhulumiwa na Benki ya Lyonnais inayomilikiwa na serikali wakati ilipoandaa mipango ya kuuzwa kwa kampuni hiyo ya vifaa vya michezo hapo mwaka 1992. Waendesha mashtaka wanamshuku Lagarde kuzifanyia ubadhirifu fedha za umma kwa sababu fedha zilizotumika kusuluhisha mzozo huo zilitoka katika hazina ya taifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO