Friday, May 24, 2013

TALIBAN WASHAMBULIA KABUL


Miripuko na milio ya risasi imesikika katikati ya Kabul leo hii wakati kundi la Taliban liliposhambulia karibu na kituo cha ujasusi na makao makuu ya kikosi cha serikali chenye kulinda makampuni ya kigeni.
Mashambulizi hayo yamekuja wiki moja baada mashambulizi mengine ya  kujitowa muhanga kwa kutumia gari lililotegwa bomu kuuwa watu 15 wakiwemo Wamarekani watano ikiwa ni shambulio baya kabisa kuwahi kushuhudiwa katika mji mkuu huo wa Afghanistan kwa takriban mwaka mmoja. Takriban mirupuko miwili ilipiga katikati ya Kabul saa nane mchana leo hii na milio ya risasi ilisikika baada ya vikosi vya usalama kukimbilia katika eneo hilo. Inaelezwa watu wenye silaha wamelikalia jengo moja na kwamba vikosi vya usalama vilikuwa vikiendelea kupambana nao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO