Friday, May 24, 2013

MAJESHI YA SYRIA YAMTIA MBARONI KAMANDA WA KUNDI LA AN NUSRA


Wanajeshi wa Syria wameua makumi ya waasi katika mapambano ya kuuokomboa mji wa kiistratijia wa Qusayr na katika maeneo tofauti ya mikoa ya Halab, Damascus na Homs.
Vikosi vya Syria aidha vimesema kuwa vimefanikiwa kumtia mbaroni kamanda wa genge la Jabhat an Nusra huko Qusayr na kuvunja jaribio la waasi hao la kuripua magari yaliyokuwa yametegwa mabomu huko Rif Dimashq na ambayo yalikuwa na karibu kilo 1300 za miripuko.
Mwandishi wa televisheni ya al Alam ameripoti kuwa jeshi la Syria limefanikiwa kuteketeza shehena kubwa ya silaha na miripuko katika eneo la kaskazini mwa mkoa wa Qusayr na kuua makumi ya waasi.
Vile vile jeshi la Syria limesema kuwa limefanikiwa kuua waasi zaidi ya 20 katika viunga vya Halab, kukamata silaha nyingi na kuteketeza makumi ya magari ya kivita ya waasi hao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO