Friday, May 24, 2013

WAPALESTINA WAANDAMANA KUPINGA SAFARI YA KERRY

Add caption

Mamia ya wananchi wa Palestina wameandamana kupinga safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni. Taarifa zinasema kuwa, Wapalestina hao wamefanya maandamano hayo katika Ukingo wa Magharibi mwa Mto Jordan sambamba na kuwazili John Kerry katika katika ukingo huo huku akipiga nara za kulaani siasa za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati na kuitaka Washington iache kuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel unaotenda jinai za kila namna dhidi ya Wapalestina.
Waaandamanaji hao pia wamewataka wakuu wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuacha kufanya mazungumzo na Wazayuni kwa sababu hayana faida zozote kwa taifa la Palestina.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO