Friday, May 31, 2013

MASHAMBULIZI YA DRONE ZA MAREKANI HUPANGWA UJERUMANI

Vyombo vya habari vya Ujerumani vimeripoti kuwa mashambulizi ya ndege za Marekani zisizokuwa na rubani barani kiafrika  yamekuwa yakiendeshwa kutoka kituo cha anga cha Ramstein kilichoko katika jimbo la Rheinland Platinate hapa Ujerumani.
Kipindi cha Panorama cha kituo cha Televisheni cha ARD, pamoja na gazeti la Süddeutsche Zeitung vimesema kuwa kituo hicho cha Ramstein ni muhimu katika kuweka mawasiliano kati ya  Marekani na ndege zake hizo wakati zikiwa kwenye mashambulizi barani Afrika.
Kwa mujibu wa gazeti la jeshi la Marekani, operesheni za ndege hizo katika nchi kama Somalia na Yemen haziwezi kufanikiwa bila kituo cha Ramstein. Serikali ya Ujerumani imesema haina habari juu ya hayo yaliyotangazwa na vyombo hivyo vya habari, kwamba mashambulizi hayo yanapangwa na kutekelezwa nchini Ujerumani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO