Friday, May 31, 2013

ASSAD YAITISHJIA ISRAEL KWA VITA MPYA

Rais wa Syria Bashar al-Assad ametishia kuanzisha upya mapambano dhidi ya Israel katika milima ya Golan, na kuongeza kuwa Urusi iko tayari kuipa nchi yake mfumo wa kisasa wa kujilinda dhidi ya mashambulizi ya anga. Akizungumza katika mahojiano na kituo cha televisheni cha cha al-Manar kinachomilikiwa na kundi la Hizbollah, Assad amesema kuna miito inayozidi kuongezeka  miongoni mwa wananchi, kutaka Syria iweke harakati mpya za kujilinda katika milima ya Golan.
Hadi sasa, Israel ambayo iliiteka milima hiyo mwaka 1981, haijatoa tamko lolote kuhusu kitisho hicho cha rais Assad. Magazeti ya Vedomosti na Kommersant  ya Urusi yamekanusha uvumi kuwa tayari Urusi imekwishaipa Syria makombora aina ya S-300, na kuongeza kuwa  huenda makombora hayo yasipelekwe Syria mwaka huu. Marekani imeonya kuwa ikiwa Urusi itaipa Syria makombora hayo, hatua hiyo itaufanya  mgogoro wa Syria kuzidi kuwa mbaya.
        

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO