Monday, May 27, 2013

MAWAZIRI WA UMOJA WA ULAYA WAGAWANYIKA JUU YA SUALA LA SYRIA

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa Umoja wa Ulaya EU wamegawanyika kuhusu mpango wa kuwaondolea vikwazo vya silaha waasi wa Syria au la, wakati huu ambapo muda makataa hiyo unafikia tamati. Licha ya mgawanyiko kushuhudiwa ndani ya mkutano ulioanza hii leo mjini Brussels Ubelgiji, mkuu wa sera za mambo ya nje wa Ulaya EU, Catherine Ashton amesema kuwa kuna matumaini makubwa ya viongozi hao kufikia muafaka. Mgawanyiko huo umedhibitishwa na waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani, Guido Westerwelle ambaye amekiri kuwa nchi nyingi za Umoja huo bado hazijaonesha wazi msimamo wao kuhusu kuwaondolea vikwazo waasi au la.
Mgawanyiko huo unatokana na hofu ya kwamba huenda mashambulizi ya mabomu ya kujitoa muhanga yanayotekelezwa nchini humo unatokana na uzagaaji wa silaha kwa upande wa waasi ambao wanatuhumiwa kushirikiana na makundi ya kigaidi nchini Syria. Hofu hiyo pia inazidi kufuatia madai ya Urusi na China kuwa waasi wa Syria wamekuwa na uhusiano na makundi ya kigaidi ambayo yanahatarisha usalama wa nchi hiyo kwakuwa silaha nyingi ziko mikononi mwa waasi. Marekani ambayo ni mshirika mkubwa kutaka kuhakikisha silaha zinatolewa kwa waasi pia imeonesha hofu yake na kudai kuwa inafikiria upya suala la kuwaondolea makataa ya silaha upande wa waasi.
Miongoni mwa nchi zinazounga mkono mkakati huo ni pamoja na Uturuki, Uingereza na Ufaransa ambazo zilikiri wazi kuwasaidia waasi kwa silaha. Kumekuwa na mazungumzo tofauti juma hili kujaribu kumaliza mzozo wa Syria huku waasi wenyewe nao wakigawanyika kuhusu uwepo wa Serikali ya Assad kwenye mazungumzo ya Geneva.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO