Sunday, May 26, 2013

MWANAJESHI APIGWA KISU PARIS

Mwanajeshi mmoja wa Ufaransa amedungwa kisu shingoni na mtu asiyejulikana alipokuwa akishika doria mjini Paris.Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema kwa hivi sasa shambulio hilo haliwezi kuhusishwa na mauaji ya mwanajeshi mjini London Uingereza yaliyotokea mapema wiki hii.Mshambuliaji huyo alitoroka baada ya kumchoma kisu Cedric Cordier mwenye umri wa miaka 23 jana jioni katika mtaa wa La Defence ambao wakati wa wikiendi hujaa watu wenye kufanya manunuzi.Afisi ya mwendesha mashitaka wa mji huo imesema wachunguzi wa kukabiliana na ugaidi watashughulikia uchunguzi wa shambulio hilo ambalo lilinaswa katika kamera.Mwanajeshi huyo aliyekuwa amevaa sare za kijeshi na alikuwa na silaha,alikuwa akishika doria kama mojawapo ya mipango ya Ufaransa ya kukabiliana na visa vya kigaidi katika maeneo muhimu ya kibiashara, usafiri na yanayotembelewa na watalii katikati mwa mji mkuu Paris.Mshambuliaji huyo ambaye  polisi wamesema ni mrefu wa mita 1.9,mwenye ndevu alikuwa amevalia fulana na suruali nyeusi alimfikia mwanajeshi huyo na kumchoma kisu na baadae kutangamana na umati bila kutamka neno lolote.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO