Sunday, May 26, 2013

ROKETI ZAJERUHI WATANO BEIRUT

Watu watano wamejeruhiwa leo wakati makombora mawili ya kurushwa kwa roketi kuripuka katika eneo linalokaliwa na Washia wengi la kusini mwa Beirut nchini Lebanon ambayo ni ngome ya kundi la Hezbollah.Roketi la kwanza lilishambulia kampuni ya kuuza magari ambapo watu wanne walijeruhiwa na magari kuharibiwa.Hii ni mara ya kwanza mji mkuu wa Lebanon Beirut kulengwa katika mzozo wa nchi jirani ya Syria ambako kundi la wanamgambo la Hezbollah linashirikiana na wanajeshi wa utawala wa Rais Bashar al- Assad kukabiliana na waasi wanaotaka kumn'goa rais huyo madarakani.Shambulio hilo la leo linakuja saa chache baada ya kiongozi wa kundi hilo la Hezbollah Hassan Nasrallah kutangaza ushindi nchini Syria.Nasrallah alikuwa akizungumza katika sherehe za kuadhimisha miaka 13 tangu kuondoka kwa majeshi ya Israel nchini Lebanon na kuongeza kuwa amekuwa akiahidi ushindi na sasa anaahidi ushindi mpya nchini Syria.Nasrallah ameapa kumuunga mkono Assad akisisitiza kuwa maslahi yao pia yako hatarini katika vita hivyo vya miaka miwili vya Syria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO