Friday, May 24, 2013

NI HARAM KUPIGANA DHIDI YA SERIKALI YA SYRIA

Khatibu wa Masjidul az Zaytuniyyah nchini Tunisia amesema kuwa, kile kinachojiri nchini Syria kwa muda wa zaidi ya miaka miwili sasa, ni njama za kutaka kuigawa nchi hiyo. Sheikh Hussein al Obeidi amesisitiza kuwa, Uislamu umeharamisha kupigana dhidi ya Waislamu. Amesema kuwa, jihadi ya uhakika ni kupambana na utawala wa Kizayuni wa Israel, utawala unaowakandamiza wananchi wa Palestina pamoja na kuyavunjia heshima matukufu ya Kiislamu huko Quds Tukufu. Sheikh al Obeidi amebainisha kuwa, haijuzu kisheria kwa Waislamu kupambana na nchi ya Kiislamu na kwamba mtu yeyote anayekwenda kupambana na wananchi wa Syria, anatenda jambo la haramu. Khatibu wa Masjidul Zaytuniyyah ameongeza kuwa, Uislamu unapinga kabisa vitendo vya kigaidi na kwamba jambo hilo liko wazi na wala halina shaka yoyote. Mwanachuoni huyo wa Tunisia amewatahadharisha vijana wa nchi hiyo wanaoelekea nchini Syria kwa shabaha ya kupambana na serikali ya Damascus na kusema kuwa, vijana hao wamekuwa wahanga wa 'kusafishwa bongo' zao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO