Friday, May 24, 2013

OBAMA, BUSH NA BLAIR WAHUKUMIWE ICC

Noam Chomsky msomi mtajika nchini Marekani amesema kuwa, Rais Barack Obama wa nchi hiyo na kiongozi aliyemtangulia George W. Bush pamoja na Tony Blair Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza wanapaswa kufikishwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC iliyoko Uholanzi, kujibu tuhuma za kutenda jinai za kivita na kibinadamu nchini Iraq kuanzia mwaka 2003. Mwandishi huyo wa Kimarekani ameongeza kuwa, Obama anahusika na jinai za kuwauwa wananchi wasio na hatia wa Pakistan, Afghanistan, Yemen na Somalia kwa kutoa ruhusa ya kutumiwa ndege zisizo na rubani dhidi ya nchi hizo, kwa kisingizio cha kupambana na makundi ya kigaidi. Matamshi ya Chomsky yanatolewa katika hali ambayo, Rais Obama hapo jana alisikika akisema kwamba, utumiwaji wa ndege hizo zisizo na rubani ni wa kisheria, kiuadilifu na wenye kuleta athari chanya kwa serikali ya Washington.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO