Sunday, May 26, 2013

UMOJA WA ULAYA WATAKIWA KULINDA ARDHI ZA PALESTINA

Kundi la mashirikia 80 ya kimataifa ya utoaji misaada limeutaka Umoja wa Ulaya EU kutekeleza ahadi zake ilizotoa mwaka uliopita za kulinda ardhi za Palestina dhidi ya mpango wa Israel wa kupanua vitongoji vya walowezi wa Kizayuni. Jumuiya ya Kimataifa ya Taasisi kwa ajili ya Maendeleo (AIDA) imesema kwamba, EU haijachukua hatua za kutosha tangu Mawaziri wa Mambo Nje wa umoja huo walipokosoa siasa za kupanuliwa vitongoji za Israel katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan mwezi Mei na kuahidi kukabiliana nazo. Kwa mujibu wa jumuiya hiyo, tangu mwezi Mei mwaka uliopita Israel imebomoa nyumba 535 za Wapalestina na majengo mengineyo yakiwemo 30 yaliyojengwa kwa msaada wa EU, na kujenga nyumba 600 za walowezi wa Kizayuni. Ripoti hiyo aidha imeongeza kwamba, kutokana na hatua hizo za Israel tangu mwaka uliopita Wapalestina wasiopungua 784 wamekosa makaazi.
Kuendelea ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu ya Palestina, kumekuwa kikwazo kikubwa cha kupatikana amani Mashariki ya Kati na kuundwa nchi huru ya Palestina.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO