Sunday, May 26, 2013

BRAZIL KUZISAMEHE MADENI YAKE NCHI ZA AFRIKA

Brazil imetangaza kuwa itazisamehe nchi za Kiafrika madeni ya karibu dola milioni 900 au kuyachunguza upya madeni hayo. Habari hiyo imetangazwa katika safari ya tatu ya Rais Dilma Rousseff wa Brazil barani Afrika ambako safari hii ameshiriki katika mkutano wa Umoja wa Afrika uliofanyika hapo jana mjini Addis Ababa Ethiopia pamoja na maadhimisho ya kuasisiwa AU. Rais Rousseff aidha amesema miongoni mwa stratejia za mambo ya nje za Brazil ni kuimarisha uhusiano maalumu na nchi za Kiafrika na kwamba nchi yake tayari imekwishashughulikia madeni yaliyokuwa yamerundikana tangu miaka ya 70. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Brazil amesema, kuangaliwa tena madeni ya baadhi ya nchi za Afrika kunamaanisha kuzingatiwa viwango bora zaidi vya riba na muda mrefu wa kulipa. Miongoni mwa nchi zitakazofaidika na suala hilo  ni Congo-Brazaville, Tanzania, Zambia, Ivory Coast, Gabon, Guinea, Guinea Bissau, Kongo DRC na Sudan.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO