Tuesday, May 28, 2013

WAFADHILI WA WAASI WA SYRIA WAKIRI JESHI LINA UWEZO MKUBWA

Nchi nyingi zinazowaunga mkono kifedha na kisilaha waasi wa Syria, zimekiri uwezo mkubwa na jeshi la nchi hiyo na kushindwa waasi katika medani ya mapambano. Mtandao wa Intaneti wa gazeti la al-Manar linalochapishwa Baytul Muqaddas umeandika kuwa, nchi nyingi ambazo hadi sasa zinawapa misaada waasi nchini Syria, zimetambua kwamba, waasi hao hawana uwezo wa kuunganisha nguvu zao wala kufikia mwafaka wa pamoja hasa katika kutafuta njia mbadala itakayoweza kuangusha serikali hahali ya Rais Bashar al-Assad wa nchi hiyo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, licha ya waasi hao kukosa makubaliano kati yao, wameshindwa pia katika uwanja wa mapambano na hivyo kushindwa kabisa kuchukua maamuzi yoyote kuhusu mustakbali wa nchi hiyo. Kwa upande mwingine, magaidi hao wamezidi kuchukiwa vikali katika jamii ya Syria, kutokana na jinai za kutisha walizozifanya dhidi ya raia wa nchi hiyo. Asilimia kubwa ya Wasyria wanaamini kuwa, waasi hao wanaooungwa mkono kutoka nje, ndio chanzo kikuu cha mgogoro na machafuko nchini mwao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO