Tuesday, May 28, 2013

WAISLAM LAGOS WAPINGA MARUFUKU YA KUVAA HIJAB NIGERIA

Wakazi wa mjini Lagos, Nigeria, wameendelea kulalamikia marufuku ya vazi takatifu la Kiislamu yaani Hijab katika shule za serikali za mjini huo. Habari zaidi zinasema kuwa, jana mitaa yote iliyo karibu na Mahakama Kuu ya mjini Lagos, ilishuhudia maandamano makubwa ya Waislamu wa mji huo wakipinga marufuku hiyo, waliyoitaja kuwa ni mwanzo wa kukanyagwa haki za Waislamu nchini Nigeria. Hivi karibuni serikali ya Abuja ilitangaza marufuku ya kuvaa Hijab katika shule za serikali za mjini Lagos. Wakati huo huo Mahakama Kuu ya mjini hapo imesema kuwa, itachunguza ombi la Waislamu, waliotaka kuondolewa marufuku hiyo mara moja. Aidha Nigeria ina jumla ya raia milioni 170 ambapo karibu nusu ya idadi hiyo inaundwa na Waislamu nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO