Thursday, May 30, 2013

WHO: PIGENI MARUFUKU MATANGAZO YA TUMBAKU KULINDA VIJANA

Shirika la afya duniani (WHO) linazitaka nchi zote duniani kupiga marufuku ya matangazo ya tumbaku ikiwemo kutokudhamini ili kulinda afya za wanadamu hasa vijana ili kupunguza idadi ya watumiaji wa bidhaa hiyo. Kupiga marufuku huko kutapunguza idadi ya vifo duniani kwani kila mwaka watu milioni 6 hufa kutokana na madhara ya tumbaku. Pia watu laki 6 amabo sio watumiaji hufa kutokana na madhara wayapatayo kutokana na moshi wa tumbaku kutoka kwa watumiaji. Nchi zilizopiga marufuku tayari zimeshashuhudia upungufu wa matumizi ya tumbaku kwa asilimia 7. Mpaka kufikia 2030 utafiti unaonesha kuwa vifo vitaongezeka kutoka milioni 6 kwa mwaka mpaka 8 ikiwa juhudi za haraka hazitochukuliwa. Dr Douglas Bettcher anasema "watumiaji wengi wa tumbaku huanza utegemezi mkubwa wa bidhaa hiyo kabla ya miaka 20" Pia Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Dr Margaret Chan anasema kuwa Nchi zote ni lazima zitoe kipaombele katika kudhibiti viwanda vya tumbaku visivyo na aibu katika kutengeneza matangazo yanayovutia yanayowarubuni hasa vijana wengi na wanawake na hatimaye kutengeneza kizazi kilichoathirika na matumizi ya nikotini.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO