Thursday, May 30, 2013

HALI YA WAISLAMU MYANMMAR BADO TETE, WAENDELEA KUUWAWA

Mwislamu moja ameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya katika hujuma mpya ya Mabudha wenye misimamo mikali dhidi ya Waislamu nchini Myanmar.Katika hujuma ya Jumanne, Mabudha waliteketeza kwa moto mali za Waislamu katika mji wa Lashio kaskazini mashariki mwa Myanmar. Kati ya sehemu zilizoteketezwa katika hujuma ya mamia ya Mabudha ni msikiti mkubwa na makao ya mayatima.  Machafuko hayo yametilia shaka madai ya serikali ya Rais Thein Sein wa Myanmar kuwa anataka kumaliza hujuma dhidi ya Waislamu waliowachache nchini humo. Karibu Waislamu 800,000 wa kabila la Rohingya nchini Myanmar wamekuwa wakikandamizwa na Mabudha wenye misimamo ya kufurutu mipaka. Mabudha hao wameteketeza kwa moto vijiji na misikiti ya Waislamu. Aidha serikali ya Myanmar inatuhumiwa kuwa imekataa makusudi kuwasaidia Waislamu hao walio wachache nchini humo. Maelfu ya Waislamu wa kabila la Rohingya wameuawa na makumi ya maelfu ya wengine kuachwa bila makao katika miezi ya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO